Saturday, April 20, 2013

AFYA JUMUISHI


Utaifa kwanza: Siku bendera ya nchi yetu ilipepea kwenye mlingoti katika 
Kitivo chetu cha Sayansi- Leiden University. Niko na Msimamizi wangu Prof. Slikerveer

Nyumbani  nikiwa na Mke wangu mwenye furaha Dr. Marja Chirangi, MD, MPH.  

Kutoka kushoto(kwako): Prof. Lionis (Ugriki), wa- Chirangi (Tanzania), Prof. Slikkerveer (Uholanzi) Prof. Joesron (Indonesia) wajumbe wa kamati ya Udaktari wa Falsafa (PhD)

Pembeni kabisa kushoto  na kulia ni Miss Judith (PhD Cand) toka Austria na Mr. Kurniawan (PhD Cand) kutoka Indonesia watu walionisindikiza kama Wapambe wa Kitaaluma (Paranymphs) kwa mujibu wa desturi za tukio hili  kwenye meza ya Utetezi wa Tasnifu 

Kushoto kwangu ni baba Mh. Prof. Muhongo ambaye pia alihudhuria na uwepo wake ulitambuliwa kipekee na Wanadhuoni  zaidi kutokana na yeye kuwa Profesa.


Hiki ndicho kitabu changu chenye Tasnifu yangu niliyoitetea yenye sura 8; kurasa 301; maneno 127,335 ambayo nimeitabaruku (dedicated) kwa Baba yetu kwa kauli ya wazi nikinena, 

This dissertation is dedicated to our beloved father, the late Mutaragara Chirangi wa Muhongo (1932 - 2007), an exemplary social, political and religious individual whose challenging legacies on innate strategic planning, efficient use of time, attention to the disadvantaged, zero tolerance on corruption, indefatigable documentation and preservation of indigenous knowledge shall continue to be evidenced in the annals of his prosopography.




 Wakati wa kusaini katika ukuta ndani ya Academy Building kuungana na wote waliowahi kuhitimu au kutunikiwa Shahada na Leiden University (Chuo cha awali Uholanzi) toka 1575 kilipoanzishwa na William, Prince of Orange. Ukutani zipo saini za akina Albert Einstein, Malkia Juliana, Malkia Beatrix, mwana wa Ufalme Willem Alexander, Nelson Mandela n.k

 

Hiki ni mojawapo ya vyumba (Senate Room) ambapo katika utamaduni na hekima ya toka enzi za mababu na mabibi katika Chuo kikuu cha Leiden watahiniwa wa uzamivu huletwa na kuulizwa maswali na jopo la wanadhuoni maprofesa kabla ya kukabidhiwa shahada za uzamivu
______________________________________

Namtukuza Mwenyezi Mungu mwenye rehema na nawashukuru Msimamizi wangu Prof. Dr. L.J.Slikkerveer, Wahadhiri wangu, Wazazi wangu, Familia yangu, Ndugu zangu, Marafiki zangu, Mwajiri wangu na Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maombi, kunipa moyo au kwa misaada yao anuwai wakati wa masomo yangu ya Udaktari wa Falsafa (Shahada ya Uzamivu).

Saa 8.00 Mchana, ya tarehe 17 Aprili 2013 nilitetea Tasnifu yangu iliyohusu:
'AFYA JUMUISHI: KUELEKEA USHIRIKIANO WA KITAALUMA KATI YA WATUMISHI WA AFYA WA TIBA YA JADI NA YA KISASA KATIKA MKOA WA MARA, TANZANIA'

Katika Ukumbi wa Kiseneta wa Chuo Kikuu cha Leiden (Leiden University), Uholanzi ambapo Mkuu wa  Chuo (Rector Magnificus) alinitunuku gombo lenye Shahada ya Uzamivu na haki zake stahiki chini ya kitivo cha Sayansi (Faculty of Science) kwa mujibu wa sheria, taratibu zihusikanazo na pia tamaduni za Taasisi za Kisomi toka hekima za enzi za mababu na mabibi .

 Tasnifu yangu ni juu ya utafiti wiani (correctional research)  ulifanyika katika Mkoa wa Mara Tanzania ambao unaolenga kuleta mabadiliko ya ki-sera katika asasi na mlimbi wa watumishi wa afya.

Zoezi hili ni kiashiria tosha cha WITO WA KUENDELEA KUWAHUDUMIA WANANCHI KWA UFANISI ZAIDI  kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu Tanzania.





Mungu ibariki Tanzania,

wa Mutaragara wa Chirangi wa Muhongo wa Nyawayega wa Rihu.