Thursday, November 26, 2009

VETERANS

SOCCER VETERANS

Mara nyingi, Ma- 'Veterans' hutumika kwa wastaafu au watu waliotumika muda mrefu katika Majeshi. Hata hivyo ni bayana kuwa jina hilo pia tunaweza kuliazima na kulitumia kuwaenzi watu waliotumikia fani za michezo.
Katika historia ya Mpira wa Miguu Tanzania, mkoa wa Mara bado haujatukuka sana ingawa katika michezo mingine kuna Timu kama vile Buhemba JKT Handball Team na Magereza Mara - Netball Team wamewahi kuutoa Mkoa Mara kimasomaso.

Aidha kuna Wachezaji na Wasanii mmoja mmoja ambao ama walitokea Mkoani Mara au wana nasaba ya watu wa Mkoani Mara  pia walionekana nyota katika kushiriki michezo na sanaa mbalimbali nchini na nje ya nchi. Hawa ni kama vile Mujaya Suleiman Nyambui (Athletic), Mahesa (Basketball); Fehadah Faru (Netball); Ali Mchumila, Lucas Jamberi, Nico Bambaga, Bite John, Castor Mumbara  (Soccer); Judith Wambura, Nyangómboli , Maringo Omwichukuru wa Kabondo-imbwa ya Salehe  (Musicians); Sele Kum-cha (Karate)- na wengine wengi ambao kamwe sitaweza kuwaorodhesha wote.

Hata hivyo tunawakumbuka na kuwaenzi wachezaji wote wakongwe waliowahi kucheza katika vilabu maarufu  vya soka huko Mara kama vile timu ya Kazi, Usagishaji, Maji, RTC,Tanesco, Mutex, Posta & Simu, Mugango, Musoma Shooting, Tarime, Seronela, Amani  na Timu machachari ya  muungano - Mara Stars.
Hapo juu ni picha ya pamoja ya baadhi ya Maveteran hao waliowahi kuchezea vilabu hivyo wakiwa katika uwanja wa Posta - Musoma (2008).

Monday, November 16, 2009

KITI CHA MAUTI




Mbele ya vipaza sauti, nje ya kituo cha kukarabati tabia cha Grerenville, Kusini mwa Richmond, sauti inasikika ikinena, “Kafa kwa amani zaidi kuliko wengi wa aliowauwa”. Hiyo ndio kauli ya Mshitaka mwakilishi wa mashahidi wa kutekelezwa kwa adhabu ya kifo (KWENYE KITI NCHA MAAUTI kwa sindano ya mauti) kwa Mdunguaji, John Allen Muhammad, aliyetuhumiwa kuua watu 10 na kusababisha hofu kuu iliyotanda jiji la Washington yapata wiki tatu, Oktoba 2002.

Historia inasema kuwa adhabu ya kifo imekuwapo kwa karne nyingi na imetolewa karibu kila kona ya dunia kwa wakosefu mbalimbali hususani waliohusika katika Uuwaji wa kukusudia, Uhaini, Usaliti (Majeshini), Ufisadi, Ukahaba na hata Ufanyaji wa biashara za madawa ya kulevya n.k kutegemeana na sheria au imani za nchi husika.
Kwa mujibu wa Amnesty International, Mwaka 2008, yapata watu 2,390 wamekufa kwa adhabu ya kifo katika nchi 25 na watu 8,864 wamehukumiwa adhabu ya kifo katika nchi 52. Tunahabarishwa kuwa Nchi zinazoongoza katika kutekeleza adhabu hii kwa mwaka 2008 ni China, Iran, Saudi Arabia, Pakistan and Marekani.
Angalau karne hii kumekuwepo na mabadiliko kiasi juu ya namna adhabu hiyo inavyotolewa katika sehemu nyingi kuliko ilivyokuwa. Hapo kale, Wanadamu waliotiwa hatiani wakahukumiwa adhabu ya kifo wame ondolewa pumzi ya uhai kwa namna mbalimbali, msisitizo ukiwa ni kufa kwa maumivu makali na au ya muda mrefu mbele ya kadamnasi ili iwe fundisho kwa wengine. Njia zilizotumika zilikuwa kama vile:-
kupigwa risari hadharani; kukoseshwa hewa kwa kufukizwa moshi au kuzamishwa majini; kuchunwa ngozi; kukatwa vipande vipande; kuchomwa moto; kuchemshwa ndani ya maji; kuchanwa vipande kwa kuvutwa na wanyama wanne;kupondwapondwa na kitu kizito sana au mnyama mzito kama Tembo; kukatwa kichwa kwa upanga; kukatwa kwa msumeno;kupigwa mawe; kusulubiwa mtini; kuachwa polini ukiwa umefungwa; kuchapwa mijeledi juu ya gurudumu la miiba; kunyongwa, kupitisha umeme mgeuko mwilini n.k.


Nadhani mabadiliko haya ya njia na hata nchi nyingine kupiga marufuku utolewaji wa adhabu hii ni zao la kukuwa kwa uelewa, mabadiliko ya kufikra, utandawazi na juhudi za Wanaharakati wa haki za Binadamu duniani kote ukiwemo Umoja wa Mataifa, Amnesty International n.k

Mjadala wa kukubali au kutokubali hukumu ya kifo ni wenye mvutano mkubwa sana duniani kwa kuwa unaibua hisia nyingi tofauti na pia kugusa imani na misimamo ya watu juu ya uhai wa Mwanadamu.

Haitoshi kusema tu kuwa malipo ya kuuwa ni kuuwawa au kwamba hakuna mwenye haki ya kuondoa uhai wa mwenziwe katika mazingira yeyote.
Hivyo kabla ya kufia uamuzi wa kuunga mkono upande fulani nashauri tutafakari bila mining’inio kwa umakini wingi na uzito wa sababu za msingi za kuunga au kutounga mkono adhabu hii ya kifo.

Aidha natoa changamoto nikiuliza kuwa;
Je tunafahamu ni wafungwa wangapi wako kwenye orodha ya kusubiri utekelezaji wa adhabu ya kifo nchini kwetu; je tunafahamu adhabu hiyo hutekelezwa wapi na kwa namna gani? Je ni vyema vyombo vya habari viwe vinafuatilia na kuruhusiwa kuhabarisha wananchi pindi mtu anapoadhibiwa au karibia kuadhibiwa hukumu ya kifo?

JUMUIYA YA WATANZANIA UHOLANZI


Picha ya pamoja ya viongozi wa Jumuiya ya Watanzania Uholanzi (TANE)


Kushoto kwa Balozi wa Tanzania - BENELUX (mwenye suti nyeusi),Mh. Mlay ni ndg. Musuto wa Chirangi aliyechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo mpya ilianzishwa juzi (14/11/2009). Jumuiya itaongozwa kwa kipindi cha 2009/10 na Mwenyekiti wake ndg. Bulemo Kweba (nyuma ya Bendera).
Viongozi wote waliochaguliwa ni :-
1. Bulemo Kweba (Chairperson)
2.
Musuto Chirangi  (Vice Chairperson)
3. Miza Mwinyimbegu (Secretary)
4. Agape Nchimbi   (Assistant Secretary)
5. Vivian Kitainda  (Treasurer)
6.
Mackfallen Anasel (Committee Member)
7.
Fanuel Karugendo (Committee Member)
8.
Mariana Josephati (Committee Member)
9.
Damian George (Committee Member)
10.
Naphtal Olemtumia (Committee Member)



Jumuiya inawaunganisha wanachama wake ambao ni Watanzania, Wenza wa Watanzania na Watoto au Wajukuu wa Watanzania wanaoishi nchini Uholanzi.


Balozi na watumishi wenzake wa ubalozi ndio walisimamia uchaguzi na kuwasimika rasmi viongozi hao.