Sunday, January 3, 2010

Kumbukumbu ya Baba Chirangi Rubhoja Bhanu









'WALIGA ULI-RUBHOJA BHANU'

Tarehe 03, Januari, 2010 inakamilisha takribani miaka mitatu tangu ututoke ghafla.
Familia yako na Wanahistoria tunaendelea kukukumbuka kwa mengi uliyotufundisha kwenye njanja mbalimbali katika Uongozi, Uadilifu na Wema wako.

Katika kumbukumbu hii, dhamira zetu leo zinaguswa zaidi na tabia yako isiyokifani ya
UKARIMU ULIOKUWA NAO KWA WATU WOTE PASI KUJALI MAKABILA, ITIKADI ZA KISIASA, IMANI, JINSI, UMRI WALA HALI ZAO ZA KIUCHUMI.

Aidha haikuwa ajali Wanadamu wakati wa ujana wako wakakupa majina ya utani kama vile Rubhoja Bhanu na pia Nyamulila Mwirango utambulisho ulioashiria tabia hii ya kukarimu watu uliyoionyesha kwa vitendo pasipo uzandiki wala masharti kwa manufaa binafsi.

Tunamuomba Mola azidi kutukumbusha nasi leo kuwakarimu wageni na wahitaji kwa jinsi tunavyoweza kuwasaidia maana kwa kufanya hivyo si tu kuwa tutakuwa tunaenzi kauli mbiu
uliyoipenda ya Haki Huinua Taifa bali pia tutakuwa tunawajibika kuwasaidia wenzetu wenye mahitaji mbalimbali kama tunavyotakiwa katika kujali utu na haki za kila Binadamu.


KWA HESHIMA NA SHUKRANI, FAMILIA YA CHIRANGI INAWASILISHA.

Friday, January 1, 2010

HERI YA MWAKA MPYA 2010







Ndugu zangu Watanzania,


Huku wengine tukiwa tumetengana kwa milima, mabonde, bahari, mipaka ya nchi na umbali mrefu na tukiwa katika mazingira tofauti kiutamaduni na kijiografia
nawatunuku nyote katika jina liletalo umoja na matumaini ya maisha.



“Mwenye matumaini hukesha usiku hadi auone mwaka mpya bali
asiye na matumaini hukesha ili kuhakikisha kuwa mwaka unapita”.

("An Optimist stays up to see the New Year in, a Pessimist waits to make sure the old one leaves ")
Ama tuwapo Watumishi au Wanafunzi, kauli hii niliyoinukuu ya busara ya
Bill Vaughan inatugusa sote ikituhasa kuwa, tunapoingia katika mwaka mpya wa 2010 tuwe watu wa matumaini.

Pasi uzandiki sote tunapewa changamoto ya kuwa na matumaini katika:

1. Kuweka mipango na kuimarisha uongozi wetu katika kazi na katika familia zetu
2. Kutoa huduma bora zaidi kwa Wateja wetu
3. Kujifunza kwa bidii stadi anuwai zenye ufanisi katika kutatua matatizo yetu
4. Kujenga na au kuboresha Umoja na Amani katika Taasisi na kwa Taifa lote.


Ninawatakieni afya njema, kila la kheri na fanaka tunapofungua sura ya kwanza na kuanza kuiandika katika hiki kitabu kipya cha 2010.


Wakatabhau,


Musuto wa- Chirangi
Utrecht, Uholanzi,