Thursday, October 29, 2015

Hongera Prof. Dkt. S. Muhongo - Mbunge Mteule


Tunampongeza Prof. Dr. Sospeter Muhongo (Ordre des Palmes Académiques), Kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Mbunge katika Jimbo la Uchaguzi la Musoma Vijijini kupitia Chama cha Mapinduzi katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25/10/2015.

Kwa uelewa na mapenzi ya wananchi wa Jimbo lake wakizingatia Kauli Mbinu yake:

 'TUKUZE UCHUMI ;TUONDOE UMASKINI PAMOJA'

Wananchi wameongea kupitia sanduku la kura.

Tunamtakia kila la kheri katika uwakilishi wa Jimbo na katika kulitumikia Taifa kwa ujumla.
Tuna imani naye katika uwajibikaji wa kweli katika kukuza uchumi kwa maendeleo ya Watanzania wote. 

Shukrani za kipekee, zimfikie Mkewe, Mama yetu, Bibi Bertha Muhongo (Msc, MBA), Timu nzima ya Kampeni na wote walioshiriki katika kufanikisha ushindi huu, hususan Wapiga Kura - Wananchi wa Musoma Vijijini. 





Saturday, October 24, 2015

SHUKRANI KWA WANANCHI: OMWAKA GWO OBHWATASYO NA IMPOKOCHOLE.


Kama ambavyo niliendelea kufanya toka tarehe 01/08/2015; naendelea kuwashukuru kupitia blogu yangu  watu  wote walioniunga mkono na hata ambao hawakuniunga mkono kwa namna moja au nyingine katika Kura za Maoni katika nafasi Ubunge Jimbo la Musoma Mjini.

Waweza sikiliza na kudadavua zaidi kwa kujikumbusha vionjo vya 'Omwaka gwo Obhwatasyo na Impokochole' hapa:










Maisha yanaendelea, hata baada ya Uchaguzi!
Tanzania Tubaki kuwa Kisiwa cha Amani! 


wa- Chirangi, PhD