Showing posts with label CCM. Show all posts
Showing posts with label CCM. Show all posts

Saturday, December 30, 2017

Asanteni Sana WanaCCM 2017





 Wanachama wa CCM;  Rafiki  na ndugu zangu;

 Asanteni sana kwa kunitia moyo na kunifanya kuwa Mgombea Uwenyekiti CCM Mkoani Mara.

"Mpira wangu waweza kuwa umegonga nguzo ya goli; lakini bado upo uwanjani ; bado upo mchezoni"

Ada ya mja hunena Muungwana ni  kitendo.  Kwa kila jambo na majira yake. Tutakiane Kheri katika mwaka mpya wa 1918.

Thursday, September 16, 2010

TUPULIZE VUVUZELA

Video: Vijanazaidi -You Tube. Shukrani kwa Kikwete 2010 Campaign Team & Michuzi:


Tanbihi: Nisemalo hapa laweza lisiwafurahishe wengine lakini linabaki kuwa kweli:

  • SANAA ILIYOUNDWA INA WELEDI WA HALI YA JUU . 
  • MAVAZI YALIYOTUMIKA NI YA HESHIMA NA YAMELANDANA NA JAMII (WANA CCM) HUSIKA PAMOJA NA SHUGHULI ILIYOPO
  • STAILI MPYA ILIYOONESHWA (KIDUKU) IMEKONGA NYOYO
  • MATUMIZI YA VUVUZELA NA RANGI ZAKE YANANYANYUA HISIA ZA MWAFRIKA KATIKA SHUGHULI ILIYOFANA HUKO BONDENI
  • MELODI YA MARLAW KAMWE HAISHAWISHI HASIRA BALI UTULIVU, MBEMBELEZO NA MGUSO WA MWILI NA ROHO
  • UCHAGUZI WA MANENO KATIKA WIMBO UNAHAMASISHA WANACHAMA NA PIA UNATUMA CHANGAMOTO KWA WANACHAMA WA VYAMA VINGINE
  • USHIRIKI WA  NGUVU WA VIJANA KWA HIYARI NA MUZIKI WA KISASA TANZANIA NI UBUNIFU NA FURSA ILIYOTUMIKA NA TIMU YA KAMPENI KWA UMAKINI KATIKA KARNE YA LEO!

WAHUSIKA WOTE WANASTAHILI PONGEZI!

NINACHOWEZA KUSHAURI TU NI KUWA,
NAFASI YA MADANSA WA KIKE INGEWEZA KUBORESHWA KWA KUWAPA MUDA WA UWIANO NA WALE WA KIUME JUKWAANI.