Friday, November 6, 2015

KILA LA KHERI, SOTE TUSHIRIKIANE KUFANYA KAZI TU!





Baada ya kula viapo stahiki, mbele ya Jaji Mkuu;tunamtakia 
Rais na Amiri Jeshi Mkuu wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt.  John Pombe Joseph Magufuli kila la kheri katika majukumu hayo makubwa na ya juu nchini kwetu. 
Aidha sote tunabaki na wito wa kuweka kando tofauti zetu na kudumisha umoja wa kitaifa huku tukifanya kazi kwa bidii na uadilifu kwa ajili ya maendeleo yetu na Taifa letu kwa ujumla.

Thursday, October 29, 2015

Hongera Prof. Dkt. S. Muhongo - Mbunge Mteule


Tunampongeza Prof. Dr. Sospeter Muhongo (Ordre des Palmes Académiques), Kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Mbunge katika Jimbo la Uchaguzi la Musoma Vijijini kupitia Chama cha Mapinduzi katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25/10/2015.

Kwa uelewa na mapenzi ya wananchi wa Jimbo lake wakizingatia Kauli Mbinu yake:

 'TUKUZE UCHUMI ;TUONDOE UMASKINI PAMOJA'

Wananchi wameongea kupitia sanduku la kura.

Tunamtakia kila la kheri katika uwakilishi wa Jimbo na katika kulitumikia Taifa kwa ujumla.
Tuna imani naye katika uwajibikaji wa kweli katika kukuza uchumi kwa maendeleo ya Watanzania wote. 

Shukrani za kipekee, zimfikie Mkewe, Mama yetu, Bibi Bertha Muhongo (Msc, MBA), Timu nzima ya Kampeni na wote walioshiriki katika kufanikisha ushindi huu, hususan Wapiga Kura - Wananchi wa Musoma Vijijini. 





Saturday, October 24, 2015

SHUKRANI KWA WANANCHI: OMWAKA GWO OBHWATASYO NA IMPOKOCHOLE.


Kama ambavyo niliendelea kufanya toka tarehe 01/08/2015; naendelea kuwashukuru kupitia blogu yangu  watu  wote walioniunga mkono na hata ambao hawakuniunga mkono kwa namna moja au nyingine katika Kura za Maoni katika nafasi Ubunge Jimbo la Musoma Mjini.

Waweza sikiliza na kudadavua zaidi kwa kujikumbusha vionjo vya 'Omwaka gwo Obhwatasyo na Impokochole' hapa:










Maisha yanaendelea, hata baada ya Uchaguzi!
Tanzania Tubaki kuwa Kisiwa cha Amani! 


wa- Chirangi, PhD

Monday, June 22, 2015

Dr. Chirangi urges Nurses to serve with competence & integrity

Musuto wa Mutaragara wa Chirangi, akiwapa Wosia Wahitimu na Wadau wa Taaluma ya Uuguzi  katika Chuo cha Sayansi za Afya - Kisare; Serengeti.