Wednesday, November 17, 2010

A New Health Centre in Musoma


Tumetangaziwa na Uongozi husika kuwa, Kituo cha Afya kipya kwa jina Bethsaida Health Centre, kilichoko katika kata ya Kigera, Manispaa ya Musoma  kinaanza kutoa huduma za Afya kwa Wananchi kuanzia 17/11/2010.





Natoa wito kwa:
  • Watumishi wa Kituo hiki kipya,  kuwa wajitahidi kutoa huduma bora isiyo aghali huku wakitii taratibu ziongozazo na maadili ya Taaluma zao kwa moyo, nguvu na akili zao zote.

  •  Uongozi wa Kituo, kutumia kanuni za Menejiment bora na Mawasiliano yenye ufanisi  huku wakijali Watumishi wao na kutathmini shughuli kila wakati ili kuboresha kiwango na ubora wa huduma kwa Wateja.

  • Manispaa yetu  na Wananchi kwa ujumla kuunga mkono juhudi hizi kwa kukubali kuwa na makubaliano ya mkataba wa utoaji huduma kwa ushirikiano wa Serikali & Sekta Binafsi  (Public - Private Partnership)  ili kuwezesha kupunguza gharama za uendeshaji na hivyo gharama za matibabu kwa Wananchi.

Sote tunamshukuru Mungu na wote waliowezesha huduma hii kuwepo.  Aidha tunamkumbuka Mzee wetu Mutaragara (RIP), mtu wa watu ambaye eneo na nyumba yake milki ndipo kituo hiki kimejengwa.


********************************************


Tuesday, November 16, 2010

Eid Mubarak!


For this pictorial, credit to: Desert Peace- nicePakistan.com



Paying Tribute to our beloved Grandma,

Kaka, Nyamurugwa wa Kafwenyi-Pili Binti Hussein(RIP),

our Uncle, Entrepreneur of the time in Musoma-township,

Rata, Juma Musuto Chirangi;(RIP)
Amri- Abeid Hse No. 21

&
Family,
Mai Nyasatu, Mai Nyamagoe (RIP)Cousins:-
Musa (RIP), Fatuma,Taabu, Mwanaisha, Said, Masatu, Meli (RIP):

I wish  all Muslims a blessing Festival of Sacrifice
(Eid al – Adha) as they commemorate the trials and triumph 
of Prophet Abraham. (Qur'an 16:120-121)

(namesake) wa- Chirangi
*******************************************************
*******************************************************

Wednesday, November 10, 2010

Tusipiganie Fito

 Picha: Kwa hisani ya Michuzi-Mzee wa Libeneke.

Uchaguzi umekwisha, Rais J.Kikwete ameshaapishwa tayari kuunda na kuongoza Serikali kwa kipindi cha miaka 5.  

Pamoja na matukio ya hapa na pale,  Mimi na familia yangu tunawapongeza Watanzania wote kwa jinsi mlivyoendeleza amani wakati wote wa Kampeni hadi kukamilika kwa Uchaguzi  Mkuu. 

Tunamwombea Rais, Makamu wake Mh. M.G.Bilal, Mawaziri na Viongozi Wengine wote wa Mihimili ya Taifa katika ngazi zote, afya njema, maono na uongozi  wenye ufanisi katika Nchi yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania.

Niliguswa sana na kauli ya "Tusigombee Fito", hivyo nami natoa mwendelezo wa wito huo kuwa :

'Shime Watanzania wote, pasi kujali tofauti zetu za ki-itikadi na vyama vyetu vya siasa, tutafute fito za kutosha na tusaidiane ili kujenga nyumba yetu kwa ushirikiano.'


Tanzania itajengwa na Watanzania Wenyewe.
Mungu ibariki Tanzania.


Wakatabhau,

Judy, Marja & Musuto wa- Chirangi

**********************************************************
**********************************************************

Kaka Umefanya Kweli!




Kaka, Godfrey Chirangi Mutaragara Chirangi wa- Muhongo wa- Nyawayega wa Rihu,

Tunakupongeza sana katika kuhitimu  kwa kufaulu  vyema Masomo ya Shahada kutoka Chuo Kikuu cha Mount Meru katika fani yako ya Ualimu na Lugha ya Kiingereza.
Mwenyezi Mungu azidi kukujalia wewe, mkeo Jane na wanao wote katika maisha. Aidha tunakuombea ili yumkini uendelee kutoa huduma bora kwa Wananchi wa Tanzania kwa ufanisi zaidi.


"Do not ask if a man has been through college; ask if a college has been through him; if he is a walking university" - Edwin Hubbell Chapin.


Ni sisi,
Judy, Marja & Musuto Chirangi 
************************************************
************************************************