Friday, January 1, 2010

HERI YA MWAKA MPYA 2010







Ndugu zangu Watanzania,


Huku wengine tukiwa tumetengana kwa milima, mabonde, bahari, mipaka ya nchi na umbali mrefu na tukiwa katika mazingira tofauti kiutamaduni na kijiografia
nawatunuku nyote katika jina liletalo umoja na matumaini ya maisha.



“Mwenye matumaini hukesha usiku hadi auone mwaka mpya bali
asiye na matumaini hukesha ili kuhakikisha kuwa mwaka unapita”.

("An Optimist stays up to see the New Year in, a Pessimist waits to make sure the old one leaves ")
Ama tuwapo Watumishi au Wanafunzi, kauli hii niliyoinukuu ya busara ya
Bill Vaughan inatugusa sote ikituhasa kuwa, tunapoingia katika mwaka mpya wa 2010 tuwe watu wa matumaini.

Pasi uzandiki sote tunapewa changamoto ya kuwa na matumaini katika:

1. Kuweka mipango na kuimarisha uongozi wetu katika kazi na katika familia zetu
2. Kutoa huduma bora zaidi kwa Wateja wetu
3. Kujifunza kwa bidii stadi anuwai zenye ufanisi katika kutatua matatizo yetu
4. Kujenga na au kuboresha Umoja na Amani katika Taasisi na kwa Taifa lote.


Ninawatakieni afya njema, kila la kheri na fanaka tunapofungua sura ya kwanza na kuanza kuiandika katika hiki kitabu kipya cha 2010.


Wakatabhau,


Musuto wa- Chirangi
Utrecht, Uholanzi,

No comments: