Sunday, January 3, 2010

Kumbukumbu ya Baba Chirangi Rubhoja Bhanu









'WALIGA ULI-RUBHOJA BHANU'

Tarehe 03, Januari, 2010 inakamilisha takribani miaka mitatu tangu ututoke ghafla.
Familia yako na Wanahistoria tunaendelea kukukumbuka kwa mengi uliyotufundisha kwenye njanja mbalimbali katika Uongozi, Uadilifu na Wema wako.

Katika kumbukumbu hii, dhamira zetu leo zinaguswa zaidi na tabia yako isiyokifani ya
UKARIMU ULIOKUWA NAO KWA WATU WOTE PASI KUJALI MAKABILA, ITIKADI ZA KISIASA, IMANI, JINSI, UMRI WALA HALI ZAO ZA KIUCHUMI.

Aidha haikuwa ajali Wanadamu wakati wa ujana wako wakakupa majina ya utani kama vile Rubhoja Bhanu na pia Nyamulila Mwirango utambulisho ulioashiria tabia hii ya kukarimu watu uliyoionyesha kwa vitendo pasipo uzandiki wala masharti kwa manufaa binafsi.

Tunamuomba Mola azidi kutukumbusha nasi leo kuwakarimu wageni na wahitaji kwa jinsi tunavyoweza kuwasaidia maana kwa kufanya hivyo si tu kuwa tutakuwa tunaenzi kauli mbiu
uliyoipenda ya Haki Huinua Taifa bali pia tutakuwa tunawajibika kuwasaidia wenzetu wenye mahitaji mbalimbali kama tunavyotakiwa katika kujali utu na haki za kila Binadamu.


KWA HESHIMA NA SHUKRANI, FAMILIA YA CHIRANGI INAWASILISHA.

2 comments:

Anonymous said...

The old chap shall be remembered always.
Rest in peace!

Anonymous said...

vijana wake naona naye wanafuata mkondo wa baba yao maana ni wachapa kazi. Kazaneni Msimwangushe mzee vijana.