Sunday, January 13, 2013

KUHUSIKA KUUWA WANANCHI NA TAIFA !


Wanahabari wote Shomy (Binda News), Marato, Mgendi, Mayunga, Cales, Bonny, Timba na wengine wote na TBC, ITV, Star TV, Victoria FM, BBC(Swahili) na vyombo vyote vya habari ingawa ni wajibu wenu, binafsi nawapongeza sana kuendelea kutuhabarisha mambo kadha wa kadha. 
Leo (jana) kuna habari zimeumiza ubongo na moyo wangu sana. Kweli sote kama wananchi tuwe macho katika mambo kama haya yanayoua Raia na Taifa kwa ujumla. Habari hizo zilikuwa ni:

1. Mauaji ya kinyama ya wananchi Mkoani kwetu (imehusisha kiongozi wetu)

2. Biashara ya meno ya tembo (ikuhusisha Askari wetu) ambayo sasa ni biashara haramu iliyoratibiwa (organized crime) na taarifa ya CNN pia imethibitisha kuwa sasa biashara hii ni zaidi ya ile madawa ya kulevya na hata zaidi ya utoroshaji haramu wa dhahabu.

3. Mfanyabiashara mwizi (si mwekezaji) wa kiwanda Dar naye akishirikiana na Mtumishi wetu (kishoka) wa TANESCO wakakwepa kulipa deni la mamilioni linalowakabili la matumizi ya umeme kwa miaka na badala yake tena wakajiungia umeme bila kupitia kwenye mita na wakaendelea kuutumia bila kuulipia wakati mwananchi wa kawaida mwenye nchi anaitafuta nishati hiyo

4. Mfanya biashara wa (Dar) kukutwa anatoa stakabadhi yenye thamani ya fedha chini ya tshs. 10,000 wakati kauza zaidi ya laki moja hivyo kukwepa kulipa kodi ambayo ni pato la Taifa kuiwezesha Serikali kutoa huduma kwa wananchi na maendeleo ya nchi yetu. Kama mnunuzi unaweza kuona jambo dogo lakini hili janga kubwa sana katika Taifa ambalo lazima sote tubadilike kama lile la matumizi mazuri ya muda.

Musuto wa- Chirangi post on facebook
Like ·  · Promote

No comments: