Saturday, February 26, 2011

TUNATOA POLE

 



TUNATOA  POLE NA FARAJA KWA FAMILIA ZILIZOPOTEZA WANAFAMILIA WAO NA WALE WOTE WALIO ATHIRIKA MOJA KWA MOJA TOKANA NA AJALI YA
MILIPUKO YA MABOMU TOKA MAGHALA YA KIKOKSI CHA JWTZ CHA 511
GONGO LA MBOTO TAREHE 16/02/2011.

WATANZANIA NA RAFIKI ZETU WOTE TUENDELEZE JUHUDI ZA 
KUTOA MISAADA MBALIMBALI KUWASAIDIA WOTE WALIOPATWA 
NA  HAYA MAAFA NA UHARIBIFU WA MALI NA WANYAMA WAO.

AIDHA NI MATUMAINI YETU KUWA, BAADA YA UCHUNGUZI KUKAMILIKA, WANANCHI WATAELEZWA TAARIFA KAMILI NA PIA HATUA MUAFAKA KUCHUKULIWA IKIWA NI PAMOJA NA ZILE ZA KUPUNGUZA MAZINGIRA HATARISHI YANAYOWEZA KUSABABISHA MILIPUKO MINGINE TENA YA NAMNA HIYO 
NA AU MADHARA KWA WANANCHI NA MALI ZAO.

Sunday, January 23, 2011

RIP Justice Mapigano

H.E, President Kikwete pays his last respect to the late Justice Dan Mapigano (RIP), retired Judge of the High Court of Tanzania; laid to rest yesterday on 19/01/2011
Familia yote ya marehemu Jaji Mapigano na rafiki yake wa karibu sana, Baba Prof. Muhongo (pichani) nawapa pole na kuwaombea faraja itokayo kwa Mola.    


(Picha kwa hisani ya Michuzi)


Monday, January 17, 2011

Maisha ya Mwanadamu Simulizi la Mola; BISEKO (RIP)




Ndg. Biseko - Master (kwenye nyota) akisikiliza kwa umakini taarifa ya Wagonjwa na Tiba katika kikao cha Asubuhi cha Watumishi wa Afya- Nyerere DDH kabla ya kuuliza maswali ambayo mara nyingi yaliibua  ama changamoto, udadisi na au utafutaji wa
utoaji Huduma bora zaidi za Afya kwa wagonjwa!
















Monday, January 3, 2011

UVUMILIVU NA SUBIRA CHANGAMOTO TOKA KWA BABA



KUMBUKUMBU (4) YA MZEE A. MUTARAGARA CHIRANGI

Pamoja na Mwanafalsafa Friesrich Nietzsche (1844 - 1900) kuona na kusema kweli kwamba, kuwa na subira au uvumilivu ni ngumu sana, hata kwa Washairi Wazamivu kushindwa kuzuia hasira zao kutoa  dhamira ya ushairi wao au kwamba shauku haitasubiri!,

 Tulimsikia na kumwona baba Mzee Mutaragara Chirangi (RIP), akionyesha uvumilivu katika anga za Siasa kwa hali isiyotegemewa.



Ni siku nyingine tena leo, ikiwa imetimia takribani miaka minne tangu atutoke duniani, tunaendelea kupata kumbukizi la changamoto toka maisha ya  huyu mzee wetu.

Katika anga za ki- Siasa hususan baada ya chaguzi, uwezo wa Binadamu wengi kuweza kuvumilia au kunyenyekea au kuonyesha subira au kujizuia kusema au kufanya jambo ambalo halina tija wala maendeleo ya mwanadamu kwa leo na kesho, ni mdogo sana.

Dhamira ya uvumilivu aliyoitangaza mzee Chirangi kwa vitendo, kamwe haikumaanisha kushindwa kudai haki au kupigia debe maisha ya kukosa misimamo, la hasha;  bali uwezo wa kutulia baada ya uchaguzi na kuchambua hali halisi na kuchukua hatua muafaka pasi jaziba,  husuda wala chuki zisizo na maana.

Wenye kumbukumbu, wanaelewa ni mara ngapi mzee huyu aliwahi kugombea nafasi mbalimbali katika njanja kadha wa kadha, akashindwa na miitikio yake ilikuwaje na hata pia ilipotokea akashinda alisema na kufanya nini kwa waliokuwa washindani au hata wapinzani wake.

Hebu tusome sehemu tu ya moja ya Hotuba zake aliyoitoa Agosti 1987,baada ya kutoa huduma kwa mfululizo wa miaka 15 kama Mwenyekiti wa CCM  Musoma mjini. Nanukuu:

Kama ambavyo nimekuwa nikisema na kutenda, ieleweke wazi kuwa kiongozi achaguliwaye kwa kutoa fedha, ataongoza kwa kuchukua fedha, vilevile achaguliwaye kwa kufuata ukabila, atasimamia kabila, naye yule achaguliwaye kwa kampeni moto toka juu huenda akaondolewa kwa kampeni baridi kutoka chini.
Aidha, ni kitendo cha kutokukomaa kisiasa, kujenga chuki na hasira kwa mtu yeyote eti kwa sababu ya kutokupigia kura, kukushinda kwenye uchaguzi au kuazimia kugombea nafasi uliyodhani umetengewa wewe pekeke”.







Japo umelala baba, sauti  na maisha yako yataendelea kutufunza milele na milele.
Kwa kila jambo kuna majira yake.....!


Musuto wa – Chirangi
Kny. Familia Yote
03/01/2011

Saturday, December 25, 2010

Merry Christmas & New Year




Wishing you all,
A Merry Christmas 
&
Prosperous New Year (2011)

Thursday, December 9, 2010

UHURU NA JAMHURI , 2010



Poster design by:  wa- Chirangi

WATANZANIA
Tunapokumbuka 
na Kushereheka 
katika Siku-kuu  ya  
Uhuru na Jamhuri - 2010,
Nawatakieni kila la kheri na fanaka. 
Aidha nawahasa pia, tutumie muda huo kutafakari 
ni jinsi gani sote mmoja mmoja au katika Kikundi / Chama / Idara/ Asasi / Wizara tunaweka Mikakati ya kuimarisha Uwajibikaji na Uzalendo katika kutoa michango yoyote chanya kwa namna yeyote  inayokubalika kwa ajili ya kujiletea
Maendeleo ya kweli ya Mtanzania 
na Tanzania kwa ujumla.


Uhuru – kazi yetu !
Uhuru – kazi yangu!

Wenu,

Musuto wa- Chirangi

Thursday, December 2, 2010

My Better Half Graduates


Blogger Templates

 My Dearest Wife,  Marja Chirangi- Schoenmeker,

Congrats for the smart work on your studies in 
Public Health: Health Services Innovations 

The family is proud of you!
May you now continue to employ all what you acquired in terms of skills, knowledge and experiences in your medical practice as well as in whatever endeavors you engage in 
as applicable while giving quality services.


Love,

 Wa- Chirangi- Omwichukuru wa Nyamurugwa wa Kafwenyi