KWA HESHIMA YA MZEE MUTARAGARA CHIRANGI ( Nyarutangwe - Omwana wa Nyamurugwa wa Kafwenyi).
ALISUKUMWA NA DHANA YA KUTENDA HAKI NA KUISHI KWA 'STD' INAYORIDHISHA.
ALIONGEA JUU YA HAKI, AKATENDA HAKI KI-STD, AKAITWA MZEE WA STD-MTETEZI WA HAKI.
NJOO TUSHAURIANE JUU YA KUBORESHA
MAISHA YETU ILI TUISHI KATIKA HAKI NA KWA STD INAYORIDHISHA
TUNATOA POLE NA FARAJA KWA FAMILIA ZILIZOPOTEZA WANAFAMILIA WAO NA WALE WOTE WALIO ATHIRIKA MOJA KWA MOJA TOKANA NA AJALI YA
MILIPUKO YA MABOMU TOKA MAGHALA YA KIKOKSI CHA JWTZ CHA 511
GONGO LA MBOTO TAREHE 16/02/2011.
WATANZANIA NA RAFIKI ZETU WOTE TUENDELEZE JUHUDI ZA
KUTOA MISAADA MBALIMBALI KUWASAIDIA WOTE WALIOPATWA
NA HAYA MAAFA NA UHARIBIFU WA MALI NA WANYAMA WAO.
AIDHA NI MATUMAINI YETU KUWA, BAADA YA UCHUNGUZI KUKAMILIKA, WANANCHI WATAELEZWA TAARIFA KAMILI NA PIA HATUA MUAFAKA KUCHUKULIWA IKIWA NI PAMOJA NA ZILE ZA KUPUNGUZA MAZINGIRA HATARISHI YANAYOWEZA KUSABABISHA MILIPUKO MINGINE TENA YA NAMNA HIYO
H.E, President Kikwete pays his last respect to the late Justice Dan Mapigano (RIP), retired Judge of the High Court of Tanzania; laid to rest yesterday on 19/01/2011
Familia yote ya marehemu Jaji Mapigano na rafiki yake wa karibu sana, Baba Prof. Muhongo (pichani) nawapa pole na kuwaombea faraja itokayo kwa Mola.
Ndg. Biseko - Master (kwenye nyota) akisikiliza kwa umakini taarifa ya Wagonjwa na Tiba katika kikao cha Asubuhi cha Watumishi wa Afya- Nyerere DDH kabla ya kuuliza maswali ambayo mara nyingi yaliibua amachangamoto, udadisi na au utafutaji wa
Pamoja na Mwanafalsafa Friesrich Nietzsche (1844 - 1900) kuona na kusema kweli kwamba, kuwa na subira au uvumilivu ni ngumu sana, hata kwa Washairi Wazamivu kushindwa kuzuia hasira zao kutoa dhamira ya ushairi wao au kwamba shauku haitasubiri!,
Tulimsikia na kumwona baba Mzee Mutaragara Chirangi (RIP), akionyesha uvumilivu katika anga za Siasa kwa hali isiyotegemewa.
Ni siku nyingine tena leo, ikiwa imetimia takribani miaka minne tangu atutoke duniani, tunaendelea kupata kumbukizi la changamoto toka maisha ya huyu mzee wetu.
Katika anga za ki- Siasa hususan baada ya chaguzi, uwezo wa Binadamu wengi kuweza kuvumilia au kunyenyekea au kuonyesha subira au kujizuia kusema au kufanya jambo ambalo halina tija wala maendeleo ya mwanadamu kwa leo na kesho, ni mdogo sana.
Dhamira ya uvumilivu aliyoitangaza mzee Chirangi kwa vitendo, kamwe haikumaanisha kushindwa kudai haki au kupigia debe maisha ya kukosa misimamo, la hasha; bali uwezo wa kutulia baada ya uchaguzi na kuchambua hali halisi na kuchukua hatua muafaka pasi jaziba, husuda wala chuki zisizo na maana.
Wenye kumbukumbu, wanaelewa ni mara ngapi mzee huyu aliwahi kugombea nafasi mbalimbali katika njanja kadha wa kadha, akashindwa na miitikio yake ilikuwaje na hata pia ilipotokea akashinda alisema na kufanya nini kwa waliokuwa washindani au hata wapinzani wake.
Hebu tusome sehemu tu ya moja ya Hotuba zake aliyoitoa Agosti 1987,baada ya kutoa huduma kwa mfululizo wa miaka 15 kama Mwenyekiti wa CCM Musoma mjini. Nanukuu:
“Kama ambavyo nimekuwa nikisema na kutenda, ieleweke wazi kuwa kiongozi achaguliwaye kwa kutoa fedha, ataongoza kwa kuchukua fedha, vilevile achaguliwaye kwa kufuata ukabila, atasimamia kabila, naye yule achaguliwaye kwa kampeni moto toka juu huenda akaondolewa kwa kampeni baridi kutoka chini.
Aidha, ni kitendo cha kutokukomaa kisiasa, kujenga chuki na hasira kwa mtu yeyote eti kwa sababu ya kutokupigia kura, kukushinda kwenye uchaguzi au kuazimia kugombea nafasi uliyodhani umetengewa wewe pekeke”.
Japo umelala baba, sauti na maisha yako yataendelea kutufunza milele na milele.
ni jinsi gani sote mmoja mmoja au katika Kikundi / Chama / Idara/ Asasi / Wizara tunaweka Mikakati ya kuimarisha Uwajibikaji na Uzalendo katika kutoa michango yoyote chanya kwa namna yeyote inayokubalika kwa ajili ya kujiletea
May you now continue to employ all what you acquired in terms of skills, knowledge and experiences in your medical practice as well as in whatever endeavors you engage in
as applicable while giving quality services.
Love,
Wa- Chirangi- Omwichukuru wa Nyamurugwa wa Kafwenyi