“…Why should my face not look sad when the city where my fathers are buried lies in ruins, and its gates have been destroyed by fire?" Nehemiah 2:3
MISINGI 10 ALIZOTUMIA MWANA DIASPORA SHUJAA
1. Kuwa na mawasiliano endelevu na nyumbani kujua si tu habari za kifamilia lakini pia maisha ya jamii na maendeleo yao kwa ujumla.
2. Kuwa na mzigo na matatizo yaliyoko nyumbani.
3. Kumshirikisha Mola katika mipango na mafanikio yetu.
4. Kutumia fursa na rasilimali tulizo nazo kwa ajili ya maendeleo ya jamii yetu
5. Kufanya tathinini za kisayansi za matatizo / mahitaji yetu halisi na kuweka mipango kazi na mikakati.
6. Kuhamasisha wengine na kugawana majukumu ikiwezekana kwa kujali vipaji / uzoefu / uwezo wetu.
7. Kushiriana pamoja kutekeleza mipango kazi.
8. Kutokuyumbishwa wala kukatishwa tamaa na wanaotubeza na au wanaotaka kutuondoa katika maono na mwelekeo wetu wa ki-maendeleo.
9. Kuonyesha ushujaa, kujilinda na ikibidi kupambana na wale wanaotaka vita na sisi.
10. Kusimamia haki, maadili na kuwajali wahitaji zaidi.
Kanuni hizi nimezinyambulisha nilipomkumbuka Kiongozi - shujaa mmoja katika Agano la kale, aliyeitwa Nehemia.
TAFADHALI KAMA HUJAWAHI SOMA AU KUTAFAKARI KWA UNDANI KITABU CHA NEHEMIA WAKATI NDIO SASA!
N.B Hata katika misaafu mingine kama Koran na hali kadhalika Hadith kuna mashujaa na wanamapinduzi wengi tu kama Nehemia.
Kwa kifupi tu ili kukupa hamu ya kusoma,
Nehemia alikuwa mshika kombe (the Cup- bearer) wa Mfalme wa Uajemi. Pamoja na kuwa katika maisha mazuri huko ughaibuni na katika hiyo kazi ya watu wachache sana katika ‘special branch’, katika kuwasiliana kwake na nyumbani, alipata habari kuwa kuta za Yerusalemu & malango yake vimebomolewa na kuchomwa moto.
Alibeba mzigo wa taabu zilizokuwa zinawakabili watu wa nyumbani Jerusalem, akahuzunika na kuomboleza sana.
Akamwomba Mola juu ya jambo hilo
Akatumia nafasi yake kumwendea Mfalme ambaye alimpa ruhusa na kumpa usalamana pia vitendea kazi vya kuanzia kazi ya ujenzi. (Sisi tunatumiaje vipawa na nafasi tulizo nazo kuendeleza jamii zetu?)
Alipofika kabla ya kuanza kazi alifanya tathmini ya kiwango cha uharibifu na kazi iliyotakiwa kufanywa na kupanga kazi.
Akahamasisha wenzake na kuwaambia kuwa tujenge pamoja, kazi iligawanywa vyema kufuata uzoefu/ uwezo. Mfano Makuhani walipewa kushughulia mlango waliouzoea na kuufahamu – mlango wa kondoo!
Watu walishirikiana wakachapa kazi mchana na usiku
Kuliibuka akina Sanbalati, Tobian na wenzao wakawabeza na kutaka kuwaondoa kazini, lakini Nehemia alisisitiza kuwa hawezi kuacha kazi.
Maadui walipopanga njama, ulinzi mkali uliwekwa na wakapambana nao. (Ni aibu sisi leo tunakatishwa tamaa wala hatupambani na maadui wetu katika maendeleo!)
Nehemia aliwasimamia haki kama kuwasaidia maskini n.k na pia akawawajibisha wakiukaji ili kulinda maadili yaliyokubalika.
Hitimisho:
Yawezekana tukawa na maisha bora zaidi popote tulipo nje ya mji au nchi, inatubidi kubeba mzigo na kuhuzunika na hali yoyote mbaya (kama ipo) katika jamii zetu. Mbele ya Viongozi wetu au Mashirika yenye uwezo au yeyote mwenye uwezo wa kutusaidia kutatua tatizo lililopo, tunapaswa kusema kuwa,
“Tutakosaje kuwa na huzuni wakati mji/ nchi ya baba zetu na mama zetu ina hali isiyoridhisha?”
Halafu tufanye kweli kwa tuchukuwa hatua 10 za kuleta maendeleo kama kiongozi wa mfano Nehemia alivyofanya.
Verbal Diarrhoea Dehydrates Human Dignity. Chirangi (2000).
KWA HESHIMA YA MZEE MUTARAGARA CHIRANGI ( Nyarutangwe - Omwana wa Nyamurugwa wa Kafwenyi). ALISUKUMWA NA DHANA YA KUTENDA HAKI NA KUISHI KWA 'STD' INAYORIDHISHA. ALIONGEA JUU YA HAKI, AKATENDA HAKI KI-STD, AKAITWA MZEE WA STD-MTETEZI WA HAKI. NJOO TUSHAURIANE JUU YA KUBORESHA MAISHA YETU ILI TUISHI KATIKA HAKI NA KWA STD INAYORIDHISHA
Friday, August 20, 2010
Tuesday, August 3, 2010
UGONJWA WA TAFSIRI NJE YA MAZINGIRA (Contextomy)
Zao la Sanaa hiyo hapo juu ni vazi-potosha liloundwa nami mwenyewe kuonyesha jinsi ugonjwa nyemelezi wa Tafsiri nje ya mazingira yake (Contextomy) unavyoweza kuwa na athari katika kupotosha umma.
Pata chanjo yake mapema kwa kutafakari jambo katika mazingira yake na katika ukamilifu wake!
Tuesday, July 20, 2010
Wahubiri katika sauti zenye Mpangilio
Kwanza Bofya kwenye play button ya Redio hapa chini usikilize.
Miziki ya kumsifu na kumtangaza Mungu imekuwepo tangu enzi za agano la kale na inaendelea kukua kwa kasi katika mapigo,ghani na staili kadha wa kadha za uchezaji wa Waimbaji.
Umuhimu wa nafasi ya muziki katika Makanisa, Misikiti na Masinagogi ni mkubwa sana katika kusaidiana na Wahubiri wengine kufikisha ujumbe kwa hadhira inayokusudiwa.
Aidha Kwaya ziimbazo au zipigazo miziki ya Kiroho pia kama walivyo mawakala wengine wa mabadiliko ya mwanadamu, zimefanya kazi kubwa ya kuwabadili, kuwafariji, kuwahubiri, kuwashawishi, kuwafundisha, kuwaonya na hata kuwapagaisha wanadamu wengi, mimi nikiwa mmoja wao!
Ukiachilia wasanii au kwaya ambazo zimeshapiga hatua kubwa, Wahubiri hawa wa sauti zenye mpangilio wanakabiliwa na changamoto nyingi, hapa chini leo nataja mbili tu:-
1. Kuhakikisha kuwa ujumbe wao unahaririwa na kupangwa vyema kabla haujawafikia hadhira. (si kujali tu mipangilio ya midundo na staili za kuruka)
2. Kurekodi kazi zao na kuwa na hati miliki. Wengi wametunga nyimbo na baada ya muda zimeachwa na kupotea tu bila kutunzwa, hapa namkumbuka Mwalimu wangu Julius Zabuloni Machumu (RIP), ambaye hadi mauti yake hakuwahi kurekodi kazi yake ya usanii iliyokuwa na ubunifu wa hali ya juu enzi hizo za miaka ya 80. Kati ya vibao vyake vilivyotikisa katika makambi ya kiroho ni Katondo tondo Maryamu Nemuka, Isaka, Kinachoshangaza, Jerusalem, Paliondokea Yohana Mbatizaji n.k
Wito:
Wadau wote tujifunge vibwebwe kuwasaidia Wahubiri hawa kwa kadiri ya uwezo wetu na vipawa vyetu maana utume wao na jumbe zao ni za muhimu sana katika maisha yetu leo na kwa vizazi vijavyo.
Hapa chini ni picha ya Mwalimu mzoefu wa Kwaya ya Upendo ya Kanisa la Mennonite Tanzania Mugumu, ndg. Gemma Igira (mwenye shati nyeupe) akiwa na Mwalimu mwenzake gwiji katika muziki wa injili ndani ya Studio yenye wapishi wa muziki waliobobea ijulikanayo kama Studio Habari Maalum Mwanza wakati waliporekodi Album ya Upendo Choir kwa jina la Tenda Miujiza. Heshima kuu kwa Waalimu wote waliotoa msaada mkubwa, Wanakwaya wote walioshiriki kutoka Jimboni kwao chini ya uongozi wa jimbo wa Mchungaji Wilson Shanyangi Machota. .
Ukipenda kujipatia nakala yako ya Album hiyo ambapo kibao hicho hapo juu (SIFUNI) kimo ndani wasiliana moja kwa moja na Uongozi wa Kwaya ya Upendo au Uongozi wa Jimbo (KMT- Mugumu c/o S.L.P 17 Mugumu, Serengeti, Tanzania au tuma barua pepe kwa gemma.igira@hotmail.com.
Miziki ya kumsifu na kumtangaza Mungu imekuwepo tangu enzi za agano la kale na inaendelea kukua kwa kasi katika mapigo,ghani na staili kadha wa kadha za uchezaji wa Waimbaji.
Umuhimu wa nafasi ya muziki katika Makanisa, Misikiti na Masinagogi ni mkubwa sana katika kusaidiana na Wahubiri wengine kufikisha ujumbe kwa hadhira inayokusudiwa.
Aidha Kwaya ziimbazo au zipigazo miziki ya Kiroho pia kama walivyo mawakala wengine wa mabadiliko ya mwanadamu, zimefanya kazi kubwa ya kuwabadili, kuwafariji, kuwahubiri, kuwashawishi, kuwafundisha, kuwaonya na hata kuwapagaisha wanadamu wengi, mimi nikiwa mmoja wao!
Ukiachilia wasanii au kwaya ambazo zimeshapiga hatua kubwa, Wahubiri hawa wa sauti zenye mpangilio wanakabiliwa na changamoto nyingi, hapa chini leo nataja mbili tu:-
1. Kuhakikisha kuwa ujumbe wao unahaririwa na kupangwa vyema kabla haujawafikia hadhira. (si kujali tu mipangilio ya midundo na staili za kuruka)
2. Kurekodi kazi zao na kuwa na hati miliki. Wengi wametunga nyimbo na baada ya muda zimeachwa na kupotea tu bila kutunzwa, hapa namkumbuka Mwalimu wangu Julius Zabuloni Machumu (RIP), ambaye hadi mauti yake hakuwahi kurekodi kazi yake ya usanii iliyokuwa na ubunifu wa hali ya juu enzi hizo za miaka ya 80. Kati ya vibao vyake vilivyotikisa katika makambi ya kiroho ni Katondo tondo Maryamu Nemuka, Isaka, Kinachoshangaza, Jerusalem, Paliondokea Yohana Mbatizaji n.k
Wito:
Wadau wote tujifunge vibwebwe kuwasaidia Wahubiri hawa kwa kadiri ya uwezo wetu na vipawa vyetu maana utume wao na jumbe zao ni za muhimu sana katika maisha yetu leo na kwa vizazi vijavyo.
Hapa chini ni picha ya Mwalimu mzoefu wa Kwaya ya Upendo ya Kanisa la Mennonite Tanzania Mugumu, ndg. Gemma Igira (mwenye shati nyeupe) akiwa na Mwalimu mwenzake gwiji katika muziki wa injili ndani ya Studio yenye wapishi wa muziki waliobobea ijulikanayo kama Studio Habari Maalum Mwanza wakati waliporekodi Album ya Upendo Choir kwa jina la Tenda Miujiza. Heshima kuu kwa Waalimu wote waliotoa msaada mkubwa, Wanakwaya wote walioshiriki kutoka Jimboni kwao chini ya uongozi wa jimbo wa Mchungaji Wilson Shanyangi Machota. .
Ukipenda kujipatia nakala yako ya Album hiyo ambapo kibao hicho hapo juu (SIFUNI) kimo ndani wasiliana moja kwa moja na Uongozi wa Kwaya ya Upendo au Uongozi wa Jimbo (KMT- Mugumu c/o S.L.P 17 Mugumu, Serengeti, Tanzania au tuma barua pepe kwa gemma.igira@hotmail.com.
Tuesday, May 25, 2010
Monday, May 17, 2010
‘Huduma za Uuguzi zinazokidhi Viwango; Wauguzi Kuongoza katika Huduma juu ya Magonjwa Sugu)’
TAFAKURI YA KAULI MBIU KWA WAUGUZI NA
WATUMISHI WENGINE WA AFYA MKOANI MARA
KATIKA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI
(INTERNATIONAL NURSES DAY) 12 MEI, 2010
‘Huduma za Uuguzi zinazokidhi Viwango;
Wauguzi Kuongoza katika Huduma juu ya Magonjwa Sugu)’
IMEANDALIWA NA KUWASILISHWA NA :
Dr. Chirangi, Bwire, (MPH)
I. Utangulizi
Wageni waalikwa Viongozi wa Serikali na Vyama vya Siasa, Viongozi wa Dini, Wawakilishi wa Mashirika mbalimbali ya Kiserikali na yasiyo ya kiserikali, Viongozi wa Chama cha Wauguzi Tanzania, Wapendwa Mashujaa wa Taaluma nyeti – Wauguzi wa Tanzania,
Paukwa…., Pakawa!
Madaktari walipokuwa wamekamilisha kazi zao, wamechoka bin taabani na kupumzika, ule wakati ambapo ukimya na giza totoro vimetawala miongoni mwa wagonjwa majeruhi vitandani, yeye aliweza kuonekana akiwa peke yake na ki-taa chake mkononi akipita kuwazungukia wagonjwa na kuwahudumia ipaswavyo..
Florence Nightingale (12 May 1820 – 13 August 1910)
Habari ndiyo hiyo, iliyoleteleza mtaalamu na shujaa - Florence Nightingale, kutambulika aka mama mwenye taa (a lady with the lamp) katika kutoa huduma ndani ya hospitali ya kijeshi (Scutari hospital) huko Uturuki wakati wa vita (Crimean War) kama ilivyonukuliwa katika gazeti (Times newspaper) la Alhamis 08 Februari 1855.
Kutokana na ushujaa wake katika kufuata wito na vipawa vyake vilipomsukuma, kutokana na moyo wake wa huruma kwa wagonjwa, kutokana na uongozi wake wa mipango, kutokana na utendaji wake wa kimaadili na usafi wa kiwango cha juu, kutokana na umahiri wake katika kutunza takwimu, kuzitafsiri na kuziwasilisha kwa ajili ya kuboresha mfumo wa afya, kutokana na kuitetea na kuiboresha taaluma ya Uuguzi, Baraza la Kimataifa la Wauguzi (The International Council of Nurses kwa kifupi ICN) liliamua tuwe tunashereheka kwa kutambua mchango mkubwa wa Wauguzi wote katika Afya na Maendeleo ya jamii zetu kwa kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya shujaa wetu Florence kila tarehe 12 Mei.
Tunaipongeza ICN kwa kazi yake makini ambapo huandaa si tu kauli mbiu ( bali pia nyenzo za utekelezaji wa kauli mbiu kwa kila mwaka. Aidha nawashukuru pia Chama cha Wauguzi Tanzania kwa kazi kubwa ya uratibu kuhusiana na maendeleo ya Taaluma ya Uuguzi na pia kutukutanisha hapa leo kama iliyo kiada, wataalamu wanapowasha ile taa na kujikumbusha kiapo cha maadili ya taaluma ya Uuguzi na zaidi ya yote kutafakari mipango mkakati juu ya mada husika ya mwaka katika maboresho ya Afya ya Mtanzania.
II. Magonjwa Sugu Utekelezaji wa Kauli Mbiu ya mwaka 2010
Mwaka huu Wauguzi wanapiga mbiu juu ya utoaji wa huduma za Uuguzi katika jamii zinazokidhi viwango na kuhakikisha kwamba Wauguzi wanashiriki kikamilifu katika huduma dhidi ya magonjwa sugu / sindika (delivering quality, serving communities:
Nurses leading chronic care)
Ndugu, Wauguzi wataalamu wenzangu katika huduma za afya, tukumbushane kuwa kwa mujibu wa takwimu za WHO (2005), magonjwa sugu kama vile Saratani, Pumu, Kiarusi, Shinikizo la Damu, Unyongofu (msongo wa mawazo), Kisukari n.k ndio yanasababisha asilimia 60% ya vifo vyote ulimwenguni.
Aidha kama tunafuata nyayo zake malaika wa huduma (the Ministering Angel)- Florence, katika kuwa makini na takwimu na kuzitumia katika kuboresha afya zetu, basi sote tutashirikiana kwa kuelimisha jamii kuwa ni hoja potofu isiyo ya kisayansi, kudhani kuwa magonjwa hayo sugu yanawakabiri zaidi watu wa nchi zenye kipato cha juu (matajiri). WHO (2005) inaonyesha takwimu za wazi kwamba 80% ya wagonjwa ni wale walio katika nchi za kipato cha chini na kati (Low & Middle income countries), hivyo Tanzania ni mojawapo!
Wengi wetu tumejifunza kwa namna moja au nyingine juu ya hayo magojwa kwa undani na tutaendelea kupata elimu juu ya matokeo ya tafiti mbalimbali kuhusu kinga, matibabu na au huduma kwa wagonjwa husika. Hapa niruhusuni nidodose tu kidog kwa nini udhibiti wa magonjwa sugu ni mada nyeti na jukumu la watu wa Mataifa yote pasi kujali utofauti wetu katika nasaba, jinsia, umri, kipato, imani wala itikadi za kisiasa .
Ni bayana Magonjwa sugu, yanatugharimu uhai wetu. bila kuchukuwa hatua, inakadiriwa kuwa jumla ya watu wapatao milioni 17 watakufa dunianii, mwaka huu kutokana na maradhi sugu.
Kwa vile magonjwa sugu ni ya muda mrefu na yenye uhitaji wa huduma za muda mrefu, maradhi haya yana madhara hasi makubwa `kwa nchi kiuchumi na kijamii. Maana yanafisha nguvu kazi katika uzalishaji na kuongeza matumizi makubwa serikali na familia husika katika kuyathibiti. Magonjwa haya yanasababisha watu kushindwa kufikia malengo yao maishani. Kuna gharama zisizo za moja kwa moja (indirect costs) kama upotezaji wa rasilimali muda makazini, mashuleni na hata majumbani n.k
Kuongezeka kwa magonjwa sugu duniani kunatokana na sababu kadha wa kadha zikiwemo ya mabadiliko ya kijamii, utandawazi, kuenea kwa maisha ya mijini (urbanization) pasipo utoshelezaji wa miundo mbinu na huduma kwa wote, kuongezeka kwa idadi ya wazee na hata ubinywaji wa haki na fursa sawa kwa wote katika mapato na huduma.
III. Utekelezaji wa Kauli Mbiu ya mwaka 2010
Kwa mujibu wa Maadili ya jumla ya Uuguzi kama yanavyoainishwa na ICN – Code of Ethics, Wauguzi wana wajibu wa msingi wa kushiriki katika kuimarisha afya na kuzuia maradhi. Aidha tunakubali kushirikiana na jamii kwa ujumla kuanzisha na kuunga mkono shughuli zinazostawisha afya na mahitaji ya kijamii ya umma.
Ndugu zangu haitoshi kutambua na kulalama juu ya changamoto mbalimbali zinazotukabili leo katika taaluma ya Uuguzi nchini. Ni vyema kwa kutumia elimu, ujuzi na umoja wetu ndani ya Chama cha Wauguzi Tanzania, Vikao vya Wauguzi na Uongozi katika Vituo vya Afya husika, Bodi za Afya za Wilaya na Mikoa na hata kupitia Kitengo cha Huduma za Uuguzi katika Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii, tuwasilishe matatizo yetu na mapendekezo yanayotukabili kwa hoja zenye takwimu rejea zilizotafsirika kisayansi kama Muasisi wetu, Meneja, Mtakwimu, Mkufunzi, Mshauri na Muuguzi mwana maboresho Florence alivyofanya katika kuipa Taaluma hadhi yake, kuwajengea uwezo Wauguzi na kuleta mapinduzi chanya ya mfumo katika huduma za Afya.
Shime, tushirikiane na wadau wote wa afya katika maeneo yetu kutekeleza Mpango Mkakati wa tatu katika sekta ya afya (the third Health Sector Strategic Plan) 2009 – 2015 ambao uko sanjari na utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (Millennium Development Goals) kufikia 2015 .
Tushirikiane kuelimisha umma juu ya vidokezo hatarishi vya magonjwa sugu na pia sisi wenyewe kama watumishi wa idara ya afya tuwe mfano (model) wa kuigwa katika familia zetu, makazini kwetu na katika jamii zetu kwa ujumla katika namna tunavyoishi kuboresha afya zetu; mfano:
Kuepuka uvutaji wa sigara / tumbaku
Kuepuka unywaji wa pombe uliokithiri
Kupata lishe bora kwa wakati muafaka
Kufanya mazoezi
Kuepuka ngono sisizo salama
Kudhibiti muendelezo wa msongo wa mawazo nk
Katika kutoa huduma husika kwa wakati muafaka kwa wagonjwa, wa magonjwa sugu, tunashauriwa kutumia CCM ( the Chronic Care Model) ambapo tunaunda mfumo:-
wenye mgojwa aliyehamasika na mwenye taarifa kamili, anayejiamini na kuweza kufanya maamuzi juu ya afya yake nauwepo wa timu ya Wataalamu ambao pia wana taarifa kamili juuu ya ugonjwa, maamuzi na mahitaji kwa ajili ya kutoa huduma kwa kiwango cha juu kwa kushirikiana na taasisi za afya.
Na pia kufuata ushauri wa WHO- ICC Framework, 2002 ( WHO-Innovative Care for Chronic Conditions , mkakati ambao pia unasisitiza kufanya maamuzi kwa rejea za takwimu, kulenga jamii husika, kuzuia ugonjwa, huduma bora iliyoratibiwa vyema,uwezo wa kuiga na kutumia kinachofaa kufuatana na mazingira husika na kuwa na ushirikiano miongoni mwa Wataalamuna na kuungwa mkono na jamii katika huduma zitolewazo.
III. Hitimisho
Ndugu Wauguzi na wageni wote waalikwa tofauti na siku kubukizi nyingi tulizonazo nchini, katika siku ya Wauguzi duniani hatukutani kwa sababu tu ya kusherehekea bali tunakutana kutafakari juu ya uratibu na utekelezaji wa mpango mkakati katika kutimiza kauli mbiu yetu ya mwaka husika.
Kwa moyo wa upendo, ninasajiri shukrani zangu za dhati kwa mchango mkubwa wa kipekee unaotolewa na Wauguzi popote walipo ulimwenguni hata ambapo Madaktari na Wataalamu wengine wanakuwa wamechoka bin taaban na giza totoro likitanda ama katika kumpunguzia mwanadamu maumivu au kurejesha na kuboresha siha yake au kumkarabati au kumtunza au kumwelimisha na kumshauri juu ya hamasa na utetezi wa maisha ya afya njema, kinga na au tiba ya maradhi.
Tutakiane kila la kheri tunapowasha taa zetu katika kuhamasisha mabadiliko chanya ya mifumo yetu na jamii kwa ujumla kuelekea huduma bora kwa wote na maisha yenye siha bora dhidi ya maradhi sugu yanayotukabili.
Sunday, January 3, 2010
Kumbukumbu ya Baba Chirangi Rubhoja Bhanu
'WALIGA ULI-RUBHOJA BHANU'
Tarehe 03, Januari, 2010 inakamilisha takribani miaka mitatu tangu ututoke ghafla.
Familia yako na Wanahistoria tunaendelea kukukumbuka kwa mengi uliyotufundisha kwenye njanja mbalimbali katika Uongozi, Uadilifu na Wema wako.
Katika kumbukumbu hii, dhamira zetu leo zinaguswa zaidi na tabia yako isiyokifani ya
UKARIMU ULIOKUWA NAO KWA WATU WOTE PASI KUJALI MAKABILA, ITIKADI ZA KISIASA, IMANI, JINSI, UMRI WALA HALI ZAO ZA KIUCHUMI.
Aidha haikuwa ajali Wanadamu wakati wa ujana wako wakakupa majina ya utani kama vile Rubhoja Bhanu na pia Nyamulila Mwirango utambulisho ulioashiria tabia hii ya kukarimu watu uliyoionyesha kwa vitendo pasipo uzandiki wala masharti kwa manufaa binafsi.
Tunamuomba Mola azidi kutukumbusha nasi leo kuwakarimu wageni na wahitaji kwa jinsi tunavyoweza kuwasaidia maana kwa kufanya hivyo si tu kuwa tutakuwa tunaenzi kauli mbiu
uliyoipenda ya Haki Huinua Taifa bali pia tutakuwa tunawajibika kuwasaidia wenzetu wenye mahitaji mbalimbali kama tunavyotakiwa katika kujali utu na haki za kila Binadamu.
KWA HESHIMA NA SHUKRANI, FAMILIA YA CHIRANGI INAWASILISHA.
Friday, January 1, 2010
HERI YA MWAKA MPYA 2010
Ndugu zangu Watanzania,
Huku wengine tukiwa tumetengana kwa milima, mabonde, bahari, mipaka ya nchi na umbali mrefu na tukiwa katika mazingira tofauti kiutamaduni na kijiografia
nawatunuku nyote katika jina liletalo umoja na matumaini ya maisha.
“Mwenye matumaini hukesha usiku hadi auone mwaka mpya bali
asiye na matumaini hukesha ili kuhakikisha kuwa mwaka unapita”.
("An Optimist stays up to see the New Year in, a Pessimist waits to make sure the old one leaves ")Ama tuwapo Watumishi au Wanafunzi, kauli hii niliyoinukuu ya busara ya
Bill Vaughan inatugusa sote ikituhasa kuwa, tunapoingia katika mwaka mpya wa 2010 tuwe watu wa matumaini.
Pasi uzandiki sote tunapewa changamoto ya kuwa na matumaini katika:
1. Kuweka mipango na kuimarisha uongozi wetu katika kazi na katika familia zetu
2. Kutoa huduma bora zaidi kwa Wateja wetu
3. Kujifunza kwa bidii stadi anuwai zenye ufanisi katika kutatua matatizo yetu
4. Kujenga na au kuboresha Umoja na Amani katika Taasisi na kwa Taifa lote.
Ninawatakieni afya njema, kila la kheri na fanaka tunapofungua sura ya kwanza na kuanza kuiandika katika hiki kitabu kipya cha 2010.
Wakatabhau,
Musuto wa- Chirangi
Utrecht, Uholanzi,
Subscribe to:
Posts (Atom)